Apr 22, 2012

WABUNGE WAZALENDO WAMETAFAKARI NA WAMECHUKUA HATUA DHIDI YA WIZI

KUONGEA SI KUTENDA ! Wabunge wazalendo wametafakari na kuchukua hatua dhidi ya wizi na ubadhirifu wa fedha za umma kwa maslahi ya Taifa. Je mbunge uliyemchagua yuko katika kundi gani?Je ana na njema na Taifa letu, Anafanya nini panapokuwa na uthibitisho kuwa mabilioni ya fedha ambayo yangesaidia kuboresha huduma za jamii yametumika kizembe au yametafunwa na waliopewa dhamana ya uongozi, Anaungana na wenzake katika kubadilisha hali hiyo au anatanguliza maslahi yake binafsi kwa sababu hakuna chama chochote ambacho kina sera ya WIZI NA UBADHIRIFU hiyo ni sera ya VIONGOZI WABINAFSI, NDULI, DHALIMU, KUPE, MAFISADI, WAOGA NA WANAFKI. Je ulipomchagua ulitegemea kumpa madaraka na cheo ili akalamike au atumie cheo chake kuboresha maisha ya watanzania , Unadhani amewajengea heshima wananchi wa jimbo lenu au amewaletea fedhea. TAFAKARI NA CHUKUA HATUA. MUNGU IBARIKI TANZANIA , MUNGU IBARIKI AFRIKA
na CG FM RADIO

No comments:

Post a Comment