Feb 15, 2012

mapenzi ni nini?

MAPENZI NI NINI?
Katika hali ya kawaida, mapenzi hayaelezeki kuwa ni nini. Ni vigumu sana mtu kukueleza maana ya mapenzi ndiyo maana kila mtu ana uelewa tofauti juu ya suala hilo.

Mtaalamu mmoja wa masuala ya mapenzi Davis Kurt kutoka Colombia, aliwahi kuyaelezea mapenzi ndani ya kitabu chake cha More About Love, ambapo alisema; ‘Love is natural feelings, which take place from the deepest part of your heart upon somebody or something else’ akimaanisha kuwa mapenzi ni hisia za asili ambazo huchukua nafasi kutoka sehemu ya ndani kabisa ya moyo juu ya mtu au kitu chochote. Tena bila kuwa na visingizio au masharti ya aina yoyote.

HISIA NI NINI?
Huu ni msukumo wa vichochezi katika homoni za ndani ya mwili ambazo hutokea kutokana na mazingira husika.
Lakini huwa tofauti kati ya mtu na mtu na ndiyo maana watu hutofautiana madaraja ya kupenda.

Mfano halisi ni kwamba, utakuta mtu anapenda sana wanawake weupe, lakini mwingine hataki hata kuwaona.
Lakini mapenzi siyo mawazo au uamuzi wa mtu, bali mapenzi ni hisia ambazo hutokea pasipo uamuzi wa mtu.

Kutokana na hali hiyo, utasikia mtu akisema ‘sijui nimempendea nini huyu mwanaume’ ni kweli yeye hajaamua lakini hisia zimefanya awe hivyo.

USIRUHUSU MAPENZI YAKUTESE
Kwa nini mapenzi yakuumize? Unakosea wapi, kwanini ukataliwe kila mara? Haya ni baadhi ya maswali ya kujiuliza kuhusu mateso ya mapenzi.

Kamwe katika maisha yako usiruhusu mapenzi yakutese, najua yawezekana kila mpenzi unayempata haudumu naye, wewe ni mtu wa kulia kila siku, hujawahi kufurahia maisha hataa siku moja, jipange upya.

Thamini na jali zaidi maisha yako kwanza, fikiria kipi ni bora kati ya mapenzi na maisha yako, ni kipi kilitangulia? Kama maisha ndiyo yalitangulia kwa nini usijijenge kwanza kimaisha ndipo mengine yafuate?

Hata kama unateswa na mtu unayempenda kwa dhati, hata kama ni mzuri kushinda malaika, kwani bila yeye maisha hayaendi? Si kweli na kama unaweza kuishi bila yeye kwa nini akutese namna hiyo?

Mpenzi msomaji wangu, hakuna kitu kinachouma kama mapenzi endapo utakosea kanauni zake, ukaruhusu moyo wote kuelekea huko, hakika yatakutesa.

No comments:

Post a Comment